Kutayarisha Njia

134/210

Sura Ya 30 - Njia Ziendazo Moyoni Zinazopaswa Kulindwa

YAFAA wote kuzilinda akili za kuona, ili Shetani asije akawashinda; maana hizi ndizo njia za rohoni. Itakubidi kuwa askari mlinzi aliye mwaminifu wa macho yako, masikio, na akili zako zote kama ukitaka kuutawala moyo wako na kuzuia mawazo mabaya yasiyofaa yasiuharibu moyo wako. Uwezo wa neema peke yake ndio uwezao kuitimiza kazi hii itakikanayo sana. KN 189.1

Shetani na malaika zake wana kazi nyingi za kufanya ya kupumbaza akili ili mashauri, maonyo, na makaripio yasisikiwe; au kama yakisikiwa, lakini yasilete matokeo mema moyoni na kuyaongoa maisha. KN 189.2