Kumjua Yesu

7/15

KUMJUA YESU

Nitwae hivi nilivyo,
Umemwaga damu yako,
Nawe ulivyoniita,
Bwana Yesu, sasa naja.

Hivi nilivyo; si langu
Kujiosha roho yangu;
Nisamehe dhambi zangu,
Bwana Yesu, sasa naja.

Nawe hivi utanitwaa;
Nisisubutu kukawa,
Na wewe hutanikataa,
Bwana Yesu, sasa naja.

Hivi nilivyo; mapenzi
Yamenipa njia wazi;
Hali na mali sisazi,
Bwana Yesu, sasa naja.
KY 60.1